Wednesday, May 29, 2013

HELAU walitimiza miaka 3 toka waanze umoja wao,  sherehe zilifanyika  January12, 2013 pale Picolo Beach Hotel. Matukio makubwa  yaliyokuwepo siku hiyo ni Mkutano Mkuu wa Mwaka, na  Fund Raising kwa ajili ya  mfuko wa kutekeleza miradi yaChama. Fuatilia matukio katika picha 

 Mkutano Mkuu wa Mwaka ulianza saa nne asubuhi ambapo ulifunguliwa na Mwenyekiti Bibi Graceana Maganga, kushoto kwake ni Bibi Hyness Mmari mwenyekiti msaidizi


 Katibu wa HELAU Bibi Eva Bugoye kulia akiwasilisha report ya mwaka, kushoto ni msaidizi wake Bibi Vesca Karigo Lwenje akihakikisha usahihi wa minutes  


                        Wajumbe /Wana kikundi/chama wa HELAU wakifuatilia Mkutano



 Bibi Agnella Meena ni Mweka Hzina wa Chama very serious anasisitiza kitu, alishidwa hata kuvaa sare she was carrying a  baby boy zilikuwa bado siku chache ajifungue lakini she managed to work for HELAU


 Ma mkubwa Bibi Joyce Pallangyo mkuu wa nidhamu akichangia mada


Viongozi wakifuatilia mada, kutoka kushoto ni Hyness na Graceana


 Wajumbe wakiwa kwenye Mkutano

Katibu  wetu Eva akisisitiza jambo 


 Mwenyekiti na Msaidizi wakipokea report toka kwa Katibu na msaidizi wake


Mweka hazina Agnella pia aliwasilisha report ya fedha akiwa na msaidizi wake Bibi Joyce Swai


Mwenyekiti na Msaidizi baada ya kupokea report zote 


Mwenyekiti akiweka mambo sawa kidigitali wakati mwenyekiti msaidizi akizungumza jambo


Muonekano wa Mwenyekiti wakati akifunga mkutano



 Baada ya Mkutano Mkuu kuisha tulipata Lunch


 Wajumbe kwenye lunchLunch, kutoka kulia ni Theresia , Herimina, na Pendo





Ulifika wakati wa tukio muhimu la Fund Raising wajumbe walibadilisha Uniform maana ilikuwa saa kumi jioni, na mkutano mkuu ulikwisha saa nane Mchana- Chezea HELAU !
Mwenyekiti alisema neno la ukaribisho kwa wageni

 Mwenyekiti Msaidizi alikuwa na neno pia 

                                                      Katibu pia alikuwa na neno
Mweka hazina  Msaidizi alikuwa na neno pia


Mwanachama Theresia kulia akiongea na baadhi ya wageni


Mgeni Rasmi kwenye Fund raising ni mwenye suti kushoto President wa SAM and ANZAI Fiber Boat Builders Co.Ltd akiingia ukumbini huku akisindikizwa na mpambe mwenye T shirt na jeans na wana HELAU wakiwa Nyuma

 Wana HELAU Kwa raha zao

 Tuli dancekwa Mbwembwe

 Wageni wetu wali dance kwa furaha

Mwenyekiti aliunganisha sala na kukaribisha wageni

 Akikaribisha wageni 

baadhi ya wageni wetu kwenye Fund raising 

 Tulikuwa na wageni wa jinsia na umri tofauti


Agnella Mweka hazina hakuwa nyuma katika kuhamasisha michango itoke pamoja na Tumbo, ama kweli mwanamke kujituma

Mweka hazina Msaidizi alihangaika na Microphone ili mradi tu Pledge zitoke hahahaaa Mwanamke ubunifu

 Katibu wetu Eva hakuchoka kuongeza chombezo kila apioona panahitaji ili kuongeza ufanisi wa kuchangia  kwa wageni 

                                                         Mwenyekiti akisema neno 

Mgeni rasmi alikabidhi Cheque yenye kiasi cha kutosha tu

 M/hazimna msaidizi Joyce Swai akirecord mahesabu

 M/kiti akisoma risala mbele ya mgeni rasmi

                                               Tulidance kwa furaha baada ya mahesabu 


 Katibu na msaidizi wake wakiyarudi

                                                     Pendo na Theresia ndani ya kiduku


 Vesva- aka -katibu msaidizi akimfuta jasho mgeni rasmi baadae ntawaeleza siri ya yeye kumfuta jasho baba huyu

Mgeni rasmi  akitoa Speech

Da Mercy akitoa pledge yake, da Mercy pia ni Mshauri wa wana HELAU

                                              Engeneer Norah naye alikuwa mgeni wetu 



                            Da Conish ni Rafiki na dada wa wana HELAU yeye alitoa Cash



 Palikuwepo na zawadi kwa wanachama Wote. tulipata Vikapu vya kubebea Documents


 Ni zamu ya Vesca kukabidhiwa zawadi ngoja tu ni waambieni ile sir ya vesca kumfuta jasho baba huyu. Jamani Mgeni rasmi ni mume wa Vesca!! tazama Pozi la Vesca anapotaka kupokea zawadi mwanamke pozi bwana
 Nasi wana HELAU pia tulimpatia Mgeni rasmi zawadi - Di Jiwe la kung'aa mithili ya diamond (Crystal) lenye maandishi ya shukrani kwake. zawadi ilikabidhiwa na mwenyekiti kwa niaba yetu

 Mgeni rasmi wetu akionesha zawadi yake - alifurahi sana - aliipenda - alikiri hakutegemea alidhani atapewa shati la batic, hahahaaaa! jamani wanawake tuwe wabunifu jamani 

 ulifika wakati wa maakuli jamani siri nyingine pia yule mpambe aliyeingia na mgeni rami ni mume wa Mwenyekiti wetu hapa mwenyekiti na mume wake wakipakua. kwa kifupi wana HELAU wote waliwaalika waume zao kuja kuchangia mfuko wa HELAU

 kutoka kushoto wanaoonekana sura ni Mume wa katibu wetu( Eva), Eva, na joyce Swai


                                        Mweka hazina msaidizi Joyce Swai akisoma report ya makusanyo(Pledges na Cash)

 Ulifuata wasaa wa kukata cake ya aniversary ambapo alibeba Mwanachama mwenye umri mdogo kuliko wote ambaye ni Vesca kuileta mezani

 Tulikata cake kwa Pamoja kuonesha sisi sote ni sawa na msingi wetu ni umoja

 na kila mmoja alijilisha

 Baadae tulikatia kwenye sahani na tuliwapatia wageni wetu kila meza iliwekwa sahani

 Norah alikuwa ni mgeni wenye umri mdogo kuliko wote naye alilishwa cake na katibu wetu Eva

 kuelekea mwisho wa shughuli mwenyekiti alitusuprise kwa kugawa zawadi kwa kila mwanachama  hapa mama kijacho Agnella anaonekana akipokea zawadi - kila mmoja  alipata zawadi ya Kidaka pochi. Kwa upendo binafsi wa Mwenyekiti 

 Nasi hatukuwa nyuma katika kumshukuru mwenyekiti na kumuonesha upendo na ushirikiano tulimtunzaje mwenyekiti!? chezea HELAU

 Mwenyekiti akijikusanyia mahela toka kwa upendo binafsi wa kila mwanachama

 Kisha tulipiga picha ya pamoja kwaajili ya kumbukumbu , tulimmiss sana mwenzetu da Rukia alikuwa ametoka kufanyiwa upasuaji muda si mrefu hivyo asingeweza kuja kurukaruka

MC alituongoza kusali sala ya kushukuru kwa mafanikio tuliyopata